Sala ya ukombozi kutoka kwa adui
Kwa mwimbishaji. Ya Daudi, kama matoleo ya ukumbusho.
1 Ee Mungu, uniokoe,
Ee BWANA, unisaidie hima.
2 Zab 109:29 Waaibike, wafedheheke,
Wanaoitafuta nafsi yangu.
Warudishwe nyuma, watahayarishwe,
Wapendezwao na shari yangu.
3 Warudi nyuma, na iwe aibu yao,
Wanaosema, Ewe! Ewe!
4 Isa 61:10;Hab 3:17;Rum 5:2;Flp 3:1;1 Pet 1:2-9 Washangilie, wakufurahie,
Wote wakutafutao.
Waupendao wokovu wako
Waseme daima, Atukuzwe Mungu.
5 Zab 40:17;Amu 5:28;Zab 141:1;Ebr 10:37;Ufu 22:20 Nami ni maskini na mhitaji,
Ee Mungu, unijilie kwa haraka.
Ndiwe msaada wangu na mwokozi wangu,
Ee BWANA, usikawie.