Wema wa Mungu na Israeli kukosa shukrani
Utenzi wa Asafu.
1 Enyi watu wangu, sikilizeni sheria yangu,
Tegeni masikio kwa maneno ya kinywa changu.
2 Nitafumbua kinywa changu kwa mithali,
Niyatamke mafumbo ya kale.
3 Mambo tuliyoyasikia na kuyafahamu,
Ambayo baba zetu walituambia.
4 Hayo hatutawaficha wana wao,
Huku tukiwaambia kizazi kingine,
Sifa za BWANA, na nguvu zake,
Na mambo yake ya ajabu aliyoyafanya.