Utukufu wa Mungu na hadhi ya utu
Kwa mwimbishaji: kwa kufuata Gitithi. Zaburi ya Daudi.
1 Ee, MUNGU, Bwana wetu
Jinsi lilivyo tukufu jina lako duniani kote!
Wewe umeuweka utukufu wako mbinguni;
2 Mt 21:16;11:25;1 Kor 1:27 Vinywani mwa watoto wachanga na wanyonyao
Umeiweka misingi ya nguvu;
Kwa sababu yao wanaoshindana nawe;
Uwakomeshe adui na mjilipiza kisasi.
3 Zab 44:16;19:1;Ayu 22:12;Rum 1:20 Nikiziangalia mbingu zako, kazi ya vidole vyako,
Mwezi na nyota ulizoziratibisha;
4 Ayu 7:17-18;Zab 144:3;Ebr 2:6-8 Mtu ni kitu gani hata umkumbuke,
Na binadamu hata umwangalie?
5 Umemfanya mdogo kuliko Mungu;
Umemvika taji la utukufu na heshima;
6 1 Kor 15:27;Efe 1:22;Ebr 2:8;Mwa 1:26 Umemtawaza juu ya kazi za mikono yako;
Umevitia vitu vyote chini ya miguu yake.
7 Kondoo, na ng’ombe wote pia;
Naam, na wanyama wa porini;
8 Ndege wa angani, na samaki wa baharini;
Na kila kipitacho njia za baharini.
9 Ayu 11:7;Zab 35:10 Wewe, MUNGU, Bwana wetu,
Jinsi lilivyo tukufu jina lako duniani kote!