Pular para o conteúdo
Publicidade

Salmos 81

Ombi la Mungu kwa Waisraeli wakaidi

Kwa mwimbishaji: kwa mtindo wa Gitithi. Ya Asafu.

1 Mwimbieni Mungu, nguvu zetu, nyimbo za furaha,

Mshangilieni Mungu wa Yakobo.

2 Pazeni zaburi, pigeni matari,

Kinubi chenye sauti nzuri, na kinanda.

3 Hes 10:10 Pigeni panda mwandamo wa mwezi,

Kukiwa na mbalamwezi, wakati wa sikukuu yetu.

4 Law 23:24;Hes 10:10 Kwa maana ni sheria kwa Israeli,

Ni hukumu ya Mungu wa Yakobo.

5 Aliamuru iwe ushuhuda katika Yusufu,

Alipoondoka juu ya nchi ya Misri;

Maneno yake nisiyemjua niliyasikia.

6 Nimeutua mzigo begani mwake;

Mikono yake nikaiondolea kazi nzito.

7 Kut 17:7;Hes 20:13 Katika shida uliniita nikakuokoa;

Nilikuitikia kutoka maficho yangu ya radi;

Nilikujaribu penye maji ya Meriba.

8 Enyi watu wangu, sikieni, nami nitawaonya,

Ee Israeli, kama ukitaka kunisikiliza;

9 Kut 20:2-3;Kum 5:6-7 Usiwe na mungu mgeni ndani yako;

Wala usimsujudie mungu mwingine.

10 Zab 37:3;Yn 15:7 Mimi ndimi BWANA, Mungu wako,

Niliyekupandisha toka nchi ya Misri;

Fumbua sana kinywa chako nami nitakijaza.

11 Lakini watu wangu hawakuisikiliza sauti yangu,

Wala Israeli hawakunitaka.

12 Mdo 7:42;Rum 1:24 Nikawaacha wakaenda kwa ukaidi wa mioyo yao,

Waenende katika mashauri yao.

13 Kum 5:29;Isa 48:18;Yer 44:4,5;Mt 23:37 Laiti watu wangu wangenisikiliza,

Na Israeli angeenenda katika njia zangu;

14 Ningewadhili adui zao kwa upesi,

Na juu ya watesi wao ningegeuza mkono wangu;

15 Wamchukiao BWANA wangenyenyekea mbele zake,

Na maangamizi yao yangedumu milele.

16 Naam, ningewalisha kwa ngano iliyo bora zaidi,

Ningewashibisha kwa asali itokayo mwambani.

Veja também