1 Njoni, tumwimbie BWANA,
Tumfanyie shangwe mwamba wa wokovu wetu.
2 Tuje mbele zake kwa shukrani,
Tumfanyie shangwe kwa zaburi.
3 Kwa kuwa BWANA ni Mungu mkuu,
Na Mfalme mkuu juu ya miungu yote.
4 Mkononi mwake zimo bonde za dunia,
Hata vilele vya milima ni vyake.
5 Bahari ni yake, ndiye aliyeifanya,
Na mikono yake iliumba nchi kavu.
6 1 Fal 8:54;1 Nya 6:13;Ezr 9:5;Dan 6:10;Lk 22:41;Mdo 7:60;1 Kor 6:20;Efe 3:14;Ayu 35:10;Isa 54:5;Yn 1:3 Njoni, tuabudu, tusujudu,
Tupige magoti mbele za BWANA aliyetuumba.
7 Ebr 3:7-11,15;4:7;Zab 95:7-11;Hes 14:22 Kwa maana ndiye Mungu wetu,
Na sisi tu watu wa malisho yake,
Na kondoo za mkono wake.
Ingekuwa heri leo msikie sauti yake!
8 Kut 17:1-7;Hes 20:2-13 Msifanye mioyo yenu kuwa migumu;
Kama ilivyokuwa huko Meriba
Kama siku ile katika Masa jangwani.
9 Hapo waliponijaribu baba zenu,
Wakanipima, wakayaona matendo yangu.
10 Ebr 3:10 Miaka arubaini nilichukizwa na kizazi kile,
Nikasema, Hawa ni watu wenye mioyo inayopotoka,
Na wanaopuuza njia zangu.
11 Hes 14:20-23;Kum 1:34-36;12:9-10;Ebr 4:3,5 Ndipo Nikaapa kwa hasira yangu
Hawataingia katika pumziko langu.