Sifa kwa utukufu wa Mungu
1 Kut 25:22 BWANA ametamalaki, mataifa wanatetemeka;
Ameketi juu ya makerubi, nchi inatikisika.
2 BWANA ni mkuu katika Sayuni,
Naye ametukuka juu ya mataifa yote.
3 Kum 28:58;Isa 6:3;Ufu 4:8 Na walisifu jina lake kuu litishalo;
Ndiye mtakatifu.
4 Kum 32:3,4;Ayu 36:5;Isa 11:3-5;Yer 23:5;Mwa 18:25 Mfalme mkuu99:4 Katika Kiebrania ni nguvu za mfalme. upendaye hukumu kwa haki;
Umeiimarisha haki;
Umefanya hukumu na haki katika Israeli.
5 1 Nya 28:2;Zab 132:7;Isa 66:1 Mtukuzeni BWANA, Mungu wetu;
Sujuduni penye kiti cha miguu yake;
Ndiye mtakatifu.
6 Musa na Haruni walikuwa makuhani wake,
Na Samweli pia ni miongoni mwa walioliitia jina lake,
Walimlilia BWANA naye akawaitikia;
7 Kut 19:9;33:9;Hes 12:5 Akasema nao katika nguzo ya wingu.
Wakashika shuhuda zake na amri aliyowapa.
8 Hes 14:20;Sef 3:7;Kum 9:20 Ee BWANA, Mungu wetu, ndiwe uliyewajibu;
Ulikuwa kwao Mungu mwenye kusamehe
Ingawa uliwapatiliza matendo yao.
9 Mtukuzeni BWANA, Mungu wetu;
Sujuduni mkiukabili mlima wake mtakatifu;
Maana BWANA, Mungu wetu, ni mtakatifu.