Pular para o conteúdo
Publicidade

Salmos 32

Shangwe kwa kusamehewa

1 Rum 4:7-8;Zab 85:2Heri aliyesamehewa dhambi,

Na kuondolewa makosa yake.

2 Law 17:4;Rum 5:13;Yn 1:47;2 Kor 1:12Heri ambaye BWANA hamhesabii hatia,

Na ambaye rohoni mwake hamna hila.

3 Nilipokosa kuungama dhambi zangu, mifupa yangu ilipooza

Kwa kulia kwangu mchana kutwa.

4 Kwa maana mchana na usiku

Mkono wako ulinilemea.

Jasho langu likakauka hata nikawa

Kama nchi kavu wakati wa kaskazi.

5 Mit 28:13;Isa 65:24;Lk 15:18Ndipo nikakuungamia dhambi yangu,

Wala sikuuficha upotovu wangu.

Nilisema, Nitayakiri maasi yangu kwa BWANA,

Nawe ukanisamehe upotovu wa dhambi yangu.

6 1 Tim 1:16;Isa 55:6;Yn 7:34Kwa hiyo, hebu kila akuaminiye

Akuombe awapo katika dhiki.

Hakika maji makuu yafurikapo,

Hayatamfikia yeye.

Veja também