3 Bali wenye haki hufurahi,
Na kuushangilia uso wa Mungu,
Naam, hupiga kelele kwa furaha.
4 Mwimbieni Mungu, lisifuni jina lake,
Mwimbieni wimbo yeye apitaye katika mawingu,
Jina lake ni YAHU;
Shangilieni mbele zake.
5 Baba wa yatima na mwamuzi wa wajane,
Ni Mungu aliye katika kao lake takatifu.