4 Kum 4:9;Kut 12:26;Yos 4:6,7Hayo hatutawaficha wana wao,
Huku tukiwaambia kizazi kingine,
Sifa za BWANA, na nguvu zake,
Na mambo yake ya ajabu aliyoyafanya.
5 Maana alikaza ushuhuda katika Yakobo,
Na sheria aliiweka katika Israeli.
Aliyowaamuru baba zetu
Wawajulishe wana wao,
6 Zab 102:18Ili kizazi kingine wawe na habari,
Ndio hao wana watakaozaliwa.
Wasimame na kuwaambia wana wao.
7 Wamwekee Mungu tumaini lao.
Wala wasiyasahau matendo ya Mungu,
Bali wazishike amri zake.