Kwa mwimbishaji: kwa mtindo wa Yungiyungi, Agano. Ya Asafu. Zaburi.
1 Kut 25:22;Kum 33:2;1 Sam 4:4;Zab 89:1 Wewe uchungaye Israeli, usikie,
Wewe umwongozaye Yusufu kama kundi;
Wewe uketiye juu ya makerubi, utoe nuru.
2 Mbele ya Efraimu, na Benyamini, na Manase,
Uziamshe nguvu zako,
Uje, utuokoe.
3 1 Fal 18:37 Ee Mungu, uturudishe,
Uangaze uso wako nasi tutaokoka.
4 Ee BWANA, Mungu wa majeshi, hadi lini
Utayaghadhibikia maombi ya watu wako?
5 Umewalisha mkate wa machozi,
Umewanywesha machozi kwa kipimo kikuu.
6 Unatufanya sababu ya ugomvi kwa jirani zetu,
Na adui zetu wanacheka wao kwa wao.
7 Ee Mungu wa majeshi, uturudishe,
Uangaze uso wako nasi tutaokoka.
8 Isa 5:1,7;Yer 2:21;Eze 15:6 Ulileta mzabibu kutoka Misri,
Ukawafukuza mataifa ukaupanda.
9 Ulitengeneza nafasi mbele yake,
Nao ukatia mizizi sana ukaijaza nchi.
10 Milima ilifunikwa kwa kivuli chake,
Matawi yake ni kama mierezi ya Mungu.
11 Kut 23:31;Zab 72:8 Nao uliyaeneza matawi yake hadi baharini,
Na vichipukizi vyake hadi kunako Mto.
12 Isa 5:5 Kwa nini umezibomoa kuta zake,
Wakauchuma wote wapitao njiani?
13 Nguruwe wa msituni wanauharibu,
Na hayawani wa kondeni wanautafuna.
14 Zek 1:12,16,17;Isa 63:15 Ee Mungu wa majeshi, tunakusihi, urudi,
Utazame toka juu uone, uujie mzabibu huu.
15 Isa 49:5 Na mche ule ulioupanda
Kwa mkono wako wa kulia;
Na tawi lile ulilolifanya
Kuwa imara kwa nafsi yako.
16 Umechomwa moto; umekatwa;
Kwa lawama ya uso wako wanapotea.
17 Zab 89:21;Kut 4:22;Zab 110:1;Dan 7:13,14;Yn 5:21-27 Mkono wako na uwe juu yake
Mtu aliye katika mkono wako wa kulia;
Juu ya mwanadamu uliyeimarisha
Kwa nafsi yako;
18 Kisha hatutakuacha kwa kurudi nyuma;
Utuhuishe nasi tutaliitia jina lako.
19 Hes 6:25;Zab 27:4,9 Ee BWANA, Mungu wa majeshi, uturudishe,
Uangaze uso wako nasi tutaokoka.