Mwito wa kuabudu na kutii
1 Njoni, tumwimbie BWANA,
Tumfanyie shangwe mwamba wa wokovu wetu.
2 Tuje mbele zake kwa shukrani,
Tumfanyie shangwe kwa zaburi.
3 Kwa kuwa BWANA ni Mungu mkuu,
Na Mfalme mkuu juu ya miungu yote.
4 Mkononi mwake zimo bonde za dunia,
Hata vilele vya milima ni vyake.
5 Bahari ni yake, ndiye aliyeifanya,
Na mikono yake iliumba nchi kavu.
6 Njoni, tuabudu, tusujudu,
Tupige magoti mbele za BWANA aliyetuumba.