8 Kut 34:6;Hes 14:18;Kum 5:10;Yak 5:11BWANA amejaa huruma na neema,
Haoni hasira upesi, ni mwingi wa fadhili.
9 Isa 57:16;Yer 3:5;Mik 7:18Yeye hatashutumu daima,
Wala hatashika hasira yake milele.
10 Ezr 9:13Hakututenda kulingana na hatia zetu,
Wala hakutulipa kwa kadiri ya maovu yetu.
11 Maana, kama mbingu zilivyoinuka juu ya nchi,
Ndivyo fadhili zake zilivyo kuu kwa wamchao.
12 Isa 43:25;Efe 1:7Kama mashariki ilivyo mbali na magharibi,
Ndivyo alivyoweka dhambi zetu mbali nasi.